Siri Ya Msalaba

 Habari Mpendwa, 

Leo tunaenda kujifunza siri iliojificha kwenye msalaba wa Yesu, ni tumaini langu kubwa utapata kitu cha kujifunza.


Yohana 3:14 Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;


Jangwani Musa alimuinua nyoka

Ilikua ni kivuli cha Yesu, Lakini jiulize kwanini mwana wa Mungu Yesu Kristo alifananishwa na nyoka

Kwanini katika wanyama wote Mungu aliamua kumfananisha na Nyoka

Tunamjua Yesu kama mwana kondoo

Lakini kwanini hasa hapa anafananishwa na nyoka yule aliyekua muerevu pale bustanini?


Ebu tumia sekunde kazaa kutafakari siri hii

Mungu alitumia mnyama yule yule anaemuwakilisha shetani pale edeni

Kumfananisha na mwanae

Lazima nitafakari sifa za nyoka

Nyoka akikungata anaacha sumu ndani yako


Sumu kazi yake kuua


Na mnajua watu wote waliong'atwa na nyoka walienda kumuangalia nyoka aliinuliwa na Musa ndipo walipopona

Sasa kama yale yalikua kivuli cha Yesu

Na kivuli kile kilikua ukingatwa na nyoka unaenda kumuangalia nyoka alie inuliwa

Ina maana kinachoangaliwa lazima kifanane na kilichokung'ata

Maana nyoka kakung'ata basi muangalie nyoka

Kwahio namuangalia Yesu msalabani kwa sababu ya kitu kilichosababishwa na aliefanana na alie msalabani

Ni kitu gani hasa kilichokua kinafanana na Yesu pale msalabani ambacho kilikua kimetudhuru sisi wanadamu ndani yetu kukawa na sumu ambayo inaleta umauti

Najua wote tunajua kua ni dhambi

Lakini je Mungu kamfananisha mwanae Yesu Kristo na dhambi?

Kwahio Yesu akiwa msalabani alikua ni nani?


Hivi ndivo biblia inavosema Yesu alikuwa nani pale msalabani


2 Wakorintho 5:21 Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.


Yeye asiyejua dhambi

Alimfanya kuwa dhambi

Kuna tofauti ya dhambi na mtenda dhambi

Yesu hakufanywa kua mtenda dhambi noo

Alifanywa kua dhambi yenyewe alivokuwa msalabani

Unazani Yesu alivokua analia pale bustanini ilikuwa ni kwasababu ya mateso ya msalaba noo 

Kwake hilo halikujalisha

Ishu iliyokua ngumu kwake ni kufanyika kuwa dhambi

Maana alijua atakavofanyika kuwa dhambi tuu

Basi Mungu Baba hapo hapo atamuacha na ni kitu ambacho Yesu hakijawahi kutokea kwake kutenganishwa na Baba yake


Ndio maana pale msalabani akalia Eloi Eloi lama sabaktani

Yani Mungu wangu mbona umeniacha?


Ni sehemu hio pekee Yesu aliliaa mbele za Mungu sehemu zote alivumilia lakini sio kuachwa na Baba


Mungu alimuacha kwasababu alikuwa dhambi 

Kwahio sio Yesu tunaemjua anasulubiwa bali ni dhambi inasulubiwa


Ebu rudi kule jangwani 

Mtu aliengatwa na nyoka 

Unazani habari njema kwake ilikua ni hipi?

Habari njema ilikuwa ni kuambiwa kua tiba ipo

Na tiba hio ndio kumuangalia Nyoka

Kwahio unapomuona Yesu msalabani lazima ujue pale alifanyika kuwa dhambi 

Kwahio pale ndo ufunuo halisi wa kwanini alifananishwa na nyoka aliyekua jangwani

Hivo Yesu pale msalabani moja ya kazi aliyoifanya

Nasema moja kwasababu msalaba umeshughulikia maeneo kadha wa kadha 

Lakini moja ya kazi kuu ni kutoa tiba ya dhambi


Unachotakiwa ni kuangalia (kuamini) tu msalaba



Hivo nyoka kwa neno hili alifananishwa na dhambi na ile sumu sasa ndio iletayo mauti na ndio matokeo ya dhambi.


Ubarikiwe kwa somo hili.

Comments

Yaliyopendwa zaidi

SIRI YA WOKOVU 1

UMENUNULIWA

NJIA TANO ZA KUFANIKIWA