Posts

Showing posts from July, 2022

UMENUNULIWA

Bwana Yesu Asifiwe!   Biblia inatufundisha jambo la msingi sana—kila aliyeokoka amenunuliwa. " Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu ." 1 Wakorintho 7:23 Hili ni suala la umiliki: Nani anakumiliki?   Kama tulinunuliwa, basi ni dhahiri kuwa kulikuwa na aliyehusika kukuuza , na kuna mwingine aliyekununua .  Hii pia inamaanisha wazi kuwa wewe si mali yako mwenyewe.  Fikiria gari— halijinunui lenyewe. Linahitaji mmiliki.  Vivyo hivyo, chochote kinachoweza kununuliwa, hakiwezi kujimiliki chenyewe.  Hili linabeba uzito mkubwa sana: Haijalishi umeokoka au hujaokoka—kila mtu yuko chini ya umiliki. Na ikiwa Mungu ndiye aliyekununua, basi kuna aliyekuuza. Na hapa ndipo tunaona ufahamu mdogo wa shetani:   Alimuuza mwanadamu pasipo kujua kuwa anapoteza kabisa haki ya umiliki Juu ya mwandamu!  Shetani alisaini mkataba huu alipomtumia Yuda kumsaliti Yesu—akidhani anashinda, kumbe anauza mali aliyokuwa anaimiliki.   Uthamani ...

KICHWA CHA KANISA

 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote. ‭‭Wakolosai‬ 1:18‬ ‭SUV‬‬ Habari Mpendwa wa Mungu, Leo tujifunze kuhusu mwili wa Kristo, Mwili wa Kristo ndio kanisa lenyewe na kanisa ni mimi na wewe, Wewe hapo ni kanisa jinsi ulivo Kichwa cha kanisa ni Yesu mwenyewe kwahio wewe kama kanisa ni mwili tu ila kichwa ni Yesu Nini maana halisi ya Kichwa cha kanisa? Kichwa ndio kina macho,mdomo,pua,masikio na ubongo(akili) Huwezi kuona,kusikia,kunusa,kuongea,k ufikiri pasipo kua na kichwa Kama Yesu ndio kichwa cha kanisa basi kanisa haliwezi kufanya hayo mambo yote pasipo Yesu. Ili uweze kutembea katika utimilifu wa Kanisa yani uweze kuenenda kama kanisa Lazima uwe na uwezo wa kujua Yesu anawaza nini, Hili ndilo la Msingi. Mfano Wewe binafsi kila kitu unachofanya haukitamki kwa mdomo wako kua unakifanya bali unakiwaza ndo unakifanya. Mfano nataka kunywa maji Ili mguu uweze ku...

SIRI YA WOKOVU 3

 Inaendelea.. Warumi 7:14  Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. Kwa maana twajua torati asilimyake ni ya rohoni Bali mimi ni mtu wa mwilini Warumi 7:5  Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za dhambi, zilizokuwako kwa sababu ya torati, zilitenda kazi katika viungo vyetu hata mkaizalia mauti mazao. Hapa anasema tulipokua katika hali ya mwili Ikidhihirisha kuwa sasa hivo hatuko katika hali ya mwili Kwahio hapa sio expirience ya paulo ambayo anapitia akiwa ndani ya wokovu noo noo Ni expirence aliokua nayo kabla hajaokoka Ndio maana kule juu alisema tulipokua katika mwili akidhihirisha kua aliempokea Yesu hayuko katka mwili Afu anasema nmeuzwa chini ya dhambi Niulize tena Hatujaona mahali amesema tumeifia torati ili tuwe mali ya mwingine? Warumi 7:4  Kadhalika, ndugu zangu, ninyi pia mmeifia torati, kwa njia ya mwili wa Kristo, mpate kuwa mali ya mwin...

SIRI YA WOKOVU 2

Inaendelea,,, Warumi 7:5  Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za dhambi, zilizokuwako kwa sababu ya torati, zilitenda kazi katika viungo vyetu hata mkaizalia mauti mazao.  Anasema tulipokuwa katika hali ya mwili Halleluyah kumbe saivi sipo katika hali yake ya mwili Paulo ametoboa siri yote hapaa Anasma tulipokua katika hali ya mwili Tamaa ya dhambii zilikuwako kwa sababu ya torati Kumbe kwanini kipindi hatujampokea Yesu tulikua tunatenda dhambi kwa fujo sana Kwasababa tamaa ya dhambi ilikuwako kwasababu ya torati Lakini sasa mimi sipo katika mwili kwahio ina maana tamaa ya dhambi haiwezi kuwako tena Inatoka wapi ? Heey Afu anasema hizo tamaa zilitenda dhambi katika viungo vyenu Kua makini anaongelea wakati ulipita sio wakati uliopo Anachomaanisha mtu aliemuamini Yesu hayupo mwilini Hivo tamaa za dhambi haziwezi kumtawala Ooh utasema mbona nmeokoka na tamaa bado zinanisumbua Haha ni kwasababu ulikua hujui ukweli huu ndo nakwambia ...

SIRI YA WOKOVU 1

 Warumi 7:1   Ndugu zangu, hamjui (maana nasema na hao waijuao sheria) ya kuwa torati humtawala mtu wakati anapokuwa yu hai? Ndugu zangu hamjui ya kua sheria inamtawala mtu akiwa hai Warumi 7:2  Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume. Anasema mwanamke akiwa ameolewa na mwanaume kuna sheria inayowafunga Mwanamke huyu akienda kwa mme mwingine wakati mme wako bado yu hai basi atakua amevunja sheria Lakini mume anapokufa huyu mwanamke ile sheria haimfungi tena Sasa utaona jinsi sheria ilivofanya kazi kwamba bila kifo sheria ilimtawala mkee Warumi 7:3  Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine. Sasa mume akiwa hai Huyu mke akienda kwa mme mwingine ni mzinzi kwasababu ya ile sheria Lakini anapokufa mme a...

NJIA TANO ZA KUFANIKIWA

  Bwana asifiwe, Kila mtu anapenda kufanikiwa, lakini tatizo limekua ni namna gani ambavyo mtu unaweza kufanikiwa. Leo nmewaandalia njia tano ambazo wewe mkristo ukifuatilia lazima uone mafanikio. Unatakiwa ujue mambo haya kwanza kabla hujafikiria jinsi ya kufanikiwa Ni mapenzi ya MUNGU kuona wewe unafanikiwa 3 YOHANA 1:2 " Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kua na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo" Ni MUNGU pia anayekupa nguvu za kuweza kufanikiwa  KUMBUKUMBU LA TORATI 8:18 " Bali utamkumbuka BWANA ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako kama hivi leo"  Baada ya kufahamu hayo sasa basi tutakwenda kuona ni vitu gani ambavo vinaweza kumfanya mkristo afanikiwe kwa kupitia mifano halisi kwenye neno la MUNGU.     1.  KUISHI VIZURI NA MUNGU Jinsi utakavoishi na kumpendeza MUNGU ndivo MUNGU atakapo kukubariki na kukuongeza zaidi na zaidi. ZABURI 1:1 "  Her...

YAKOBO NA ISRAELI

 Isaya 48:12 Nisikilize mimi, Ee Yakobo; na Israeli, niliyekuita; mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho pia. Mstari huu tunaona situation Mungu akitaka attention ya mtu lakini anamuita kwa majina mawili Jina la kwanza anamuita yakobo alafu anamuita israel Utashangaa kujua kua Mungu mwenyewe alimbadilisha jina Yakobo kua Israel na akamwambia kwanzia leo hutoitwa kwa jina la yakobo Mwanzo 32:28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda. Kwahio Mungu mwenyewe alisema kua hatoitwa tena yakobo Hii inatuonyesha kua ujumbe huu anaoutoa yamkini umesababishwa na yakobo na israel Au kwa tafsiri nyingine umesababishwa na tabia za kale za israel Ikiwa na maana Yakobo tabia za ukale Maana tafsiri ya neno jina ni tabia Kwahio akimuita mtu kwa jina la zamani ina maana bado anaona kuna tabia za zamani bado zipo ndani ya huyo mtu. Au niseme hivi kama israel amebadilishwa jina Ukiitwa kwa jina la za...

NGOME ZA KUANGUSHA

  2 Wakorintho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) Biblia inasema silaha za vita vyetu si za mwili. Kwahio tujue mpaka hapo tupo kwenye vita Maana hatuwezi tukawa tunaongelea kuhusu maswala ya silaha za vita wakati hatuna vita Kwahio hapo nikukujulisha kua tupo kwenye vita. Lakini pia ni kukujulisha kua hio vita haitumii silaha unazozijua hizi za mwili Yani bunduki,mabomu nk Ila zinauwezo katika Mungu, Kwa tafsiri rahisi hizo silaha zimetengenezwa na Mungu Na kila silaha inauwezo wake Tunajua kuna bunduki ina uwezo wake Kuna short gun pia kuna sniper hizi zote ni silaha lakini zinauwezo tofauti Hivo nategemea kuona silaha hizi ambazo zina uwezo katika Mungu zinauweza wake Na kutokana huu mstari tunajulishwa hizo silaha zinauwezo kiasi kwamba zinaweza kuangusha ngome Ngome ni majumba yaliojengwa kwa ufasaha ambayo ukuta wake ni mgumu na ni imara sana sio rahisi uanguke Kwahio hizo silaha...

WAMGOJEAO BWANA

  Isaya 40:31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia. Ebu vuta hisia zako uko mahali unamgojea mtu. Afu jiulize unamgojea aje kufanya nini? Je una appointment nae? Kwa maswali haya tu ni dhahiri kabisa hauwezi kumngojea mtu kama hamjapanga mkutane mahali au kama hajakwambia umsubiri mahali. Biblia inasema wamngojeao Bwana Tujiulize kwanini unamgojea Bwana, je una appointment yeyote na yeye, Je amekwambia umsubirie labda akuletee kitu. Ebu tafakari unamgojea Bwana afanyaje? Usije ukawa unamgojea wakati yeye hana taarifa yeyote kwamba unamgojea Kwahio ili ufike hatua ya kumngojea mtu lazima pande zote mbili ziwe na taarifa Yamkini kuna kitu umemuomba Mungu Akasema subiri Basi wewe unatakiwa umngojee Bwana. Mungu akikuahidi jambo lazima ujifunze kumngojea hadi pale atakapotimiza Ili uweze kumngojea Bwana Anza kwa kumsikiliza yeye, ...

ROHO NA MWILI

 Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu,kwa sura yetu Hii lazima ikupe maswali kua Mungu anafananaje? Biblia inatupa majibu kua Mungu anafananaje. Yohana 4:24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli Biblia inasema Kua Mungu ni roho Hivo basi Mungu akisema tumfanye mtu kwa mfano wetu na kwasura yetu basi hapo tunajua kua Mungu anamfanya mtu ambae ni roho na yeye Ila huyo mtu ambae ni Roho kuna dhumuni kuu aliloumbiwa Aliumbwa ili atawale, Mungu baada ya kuumba kila kitu akataka mtawala na huyo mtawala alitaka afanane nae Kwahio Mungu akamfanya mtu ambae ni Roho Mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake Mwanaume na mwa...

HATUA KATIKA KUITWA

 Kutoka 3:2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. Yamkini una wito ndani yako na labda unajua kua Mungu amekuita kwa ajili ya kitu fulani. Mungu akikuita ujue kuna maagizo anataka uyatekeleze, Mungu hatokuita tu ilimradi tu uokoke afu uwe unaenda kanisani na kurudi iishie hapo, kuna zaidi ya hapo, kuna kusudi maalumu kabisa ambalo anataka yeye alifanikishe hapa duniani na ili alifanikishe anaona ni vema akutumie wewe. Wito sio kua mchungaji,mwalimu,nabii au mtume peke yake Kazi yako inaweza ikawa wito wako pia. Kupitia hio kazi Kuna vitu Mungu anataka kuvifanikisha hapa duniani. Kuna hatua katika wito wako,zifuatazo ndio hatua za kuendea wito wako. 1- KUSHUHUDIA MATENDO MAKUU Hatua ya kwanza katika Mungu kukutafuta wewe hua anakupa kibali cha wewe kushuhudia matendo makuu yakitendeka mbele ya macho yako,utaona watu wakiponywa,utaona miujiza ya ...

Siri Ya Msalaba

 Habari Mpendwa,  Leo tunaenda kujifunza siri iliojificha kwenye msalaba wa Yesu, ni tumaini langu kubwa utapata kitu cha kujifunza. Yohana 3:14 Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa; Jangwani Musa alimuinua nyoka Ilikua ni kivuli cha Yesu, Lakini jiulize kwanini mwana wa Mungu Yesu Kristo alifananishwa na nyoka Kwanini katika wanyama wote Mungu aliamua kumfananisha na Nyoka Tunamjua Yesu kama mwana kondoo Lakini kwanini hasa hapa anafananishwa na nyoka yule aliyekua muerevu pale bustanini? Ebu tumia sekunde kazaa kutafakari siri hii Mungu alitumia mnyama yule yule anaemuwakilisha shetani pale edeni Kumfananisha na mwanae Lazima nitafakari sifa za nyoka Nyoka akikungata anaacha sumu ndani yako Sumu kazi yake kuua Na mnajua watu wote waliong'atwa na nyoka walienda kumuangalia nyoka aliinuliwa na Musa ndipo walipopona Sasa kama yale yalikua kivuli cha Yesu Na kivuli kile kilikua ukingatwa na nyoka unaenda kumuangalia n...