UTAMBUE NA UTAMKE UUNGU WAKO-Rapsodi ya uhakika Jumatatu 16 August
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele (Yohana 3:16). M stari wetu wa ufunguzi si ahadi; ni sheria. Ni kama tu vile 2 Wakorintho 5:17. “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.” Huu na mstari wetu wa ufunguzi si ahadi za kutoka kwa Mungu; ni matamko ya kifalme toka kwa Mungu. Yule aliyezaliwa tena ni kiumbe kipya; anao uzima na asili ya Mungu. Kuwa umezaliwa tena, uhai wako wa kibinadamu ulimezwa na uzima na asili ya Mungu. Sasa, mwili wako unafunika aina mpya ya uzima ambao hauingiliki wala kufikiwa na maradhi au magonjwa. Mambo ya kale yamepita; tazama, mambo yote yamekuwa mapya! Kama haujui kuhusiana na uzima huu mpya, kamwe hautauweka katika matendo; utakuwa ukiishi maisha ya kibinadamu angali una uzima wa kiungu ndani yako. Jifunze kuuchochea uzima wa kiungu ndani yako, kwa kutamka na ...