SIRI YA WOKOVU 3
Inaendelea..
Warumi 7:14
Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.
Kwa maana twajua torati asilimyake ni ya rohoni
Bali mimi ni mtu wa mwilini
Warumi 7:5
Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za dhambi, zilizokuwako kwa sababu ya torati, zilitenda kazi katika viungo vyetu hata mkaizalia mauti mazao.
Hapa anasema tulipokua katika hali ya mwili
Ikidhihirisha kuwa sasa hivo hatuko katika hali ya mwili
Kwahio hapa sio expirience ya paulo ambayo anapitia akiwa ndani ya wokovu noo noo
Ni expirence aliokua nayo kabla hajaokoka
Ndio maana kule juu alisema tulipokua katika mwili akidhihirisha kua aliempokea Yesu hayuko katka mwili
Afu anasema nmeuzwa chini ya dhambi
Niulize tena
Hatujaona mahali amesema tumeifia torati ili tuwe mali ya mwingine?
Warumi 7:4
Kadhalika, ndugu zangu, ninyi pia mmeifia torati, kwa njia ya mwili wa Kristo, mpate kuwa mali ya mwingine, yeye aliyefufuka katika wafu, kusudi tumzalie Mungu matunda.
Hapa alisema kadhalika ndugu zangu mmeifa torati kwa njia ya mwili wa Kristo mpate kua mali ya Mwingine
Warumi 7:14
Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.
Hapa anasema nmeuzwa chini ya dhambi
Utagundua hapa anaongelea kwa habari ya kipindi ambacho bado hajampokea Yesu
Kua hapa haongelei maisha ya Mkristo aliyeokoka bali mtu ambae hajaokoka
Warumi 7:15
Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda.
Huyu mtu ambaye anatenda hivo ni mtu ambaye hajaokoka sio wewe ulioifia torati
Ooh mbona nahisi kama hili neno linaniongelea mimi kabisa
Mbona vitu navofanya sivitaki
Well ulikua hujui tu ila sasa nmekupa ukweli huu anza kukiri sawa sawa na neno linavosema
Ni sawa na mtu anaeumwa
Afu neno linasema hauumwi unaamini nini?
Una amini hisia za mwili wako au neno
Wewe upo rohoni hata kama unajihisi haupo hizo ni hisia zako lakini neno linasema tuliofia torati hatupo katika mwili
Kwahio acha hizi habari za kukiri hili neno vibaya
Nmechagua kuamini neno la Mungu nasio hali au mazingira yangu
Neno la Mungu ni kioo
Nikilisoma najiona mimi nilivo
Sisahau kile nilichokiona kwenye neno
Maana nikisahau ni sawa na mtu anaejiangalia kwenye kioo afu akiondoka anasahau sura yake ikoje
Kama neno ni kioo ukiangalia unajiona
Neno linavosema wewe upo rohoni ujue neno linakuonyesha uhalisia wako uliokua huujui
Warumi 7:17
Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
Mkristo ulieokoka unaweza kuchukua hili neno nakusema eti sio mimi ni dhambi ndani yangu
Dhambi gani?
Yesu alifanyika kua dhambi hivo dhambi ilisulubiwa msalabani
Ni ukosefu wa maarifa ya kimungu kujiita kuwa yeye ni mwenye dhambi
Mkristo anaweza kutenda dhambi kwa kutaka
Lakini haimaanishi yeye ni mwenye dhambi
Kibiblia mwenye dhambi ni yule ambaye hajampokea Yesu
Warumi 7:24
Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?
Ooh paulo ashukuriwe Yesu mwokozi alikua kutuokoa na mwili huu wa mauti
Ndio maana mstari unaofuata anasema
Warumi 7:25
Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.
Anamshukuru Mungu wa Bwana Yesu kwasababu ya wokovu aliolutea
Ubarikiwe kwa somo hili!!
Comments
Post a Comment